Breaking




Sunday, 17 September 2017

KINSHASA YAANZISHA UCHUNGUZI BAADA YA KUUAWA KWA WAKIMBIZI 34 KUTOKA BURUNDI

Sungo blog

Serikali ya Kinshasa yafahamisha kuanza uchunguzi baada ya kuuawa kwa wakimbizi 34 kutoka Burundi Kamanyola

Serikali ya Kinshasa yatangaza kuanza uchunguzi kufuatia vifo vya wakimbizi 34 kutoka nchini Burundi waliouawa kwa kupigwaa risasi Kamanyola Mashariki mwa Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo.

Kwa upande wake serikali ya Bujumbura  iliitaka seriakali ya Kinshasa na Umoja wa Mataifa kutoa maelezo kuhusu tukio hilo.

Msemaji wa serikali ya Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo Lambert Mende amefahamisha kuwa serikali imeanzisha uchunguzi Jumamosi baada ya wakimbizi kufyatuliwa risasi Mashariki mwa DR Congo.

Taarifa zafahamishakuwa wanajeshi  watano waliuawa na watu wanaodaiwa kuwa wakimbizi jambo ambalo linashangaza serikali ya DR Congo vipi wakimbizi wanaweza kuwa na silaha na kushambulia

No comments:

Post a Comment