Breaking




Monday, 11 September 2017

ZAIDI YA WANANCHI 11,000 WAJITOKEZA KUPIMA AFYA

Sungo blog

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam,Paul Makonda jana amefunga rasmi zoezi la Siku tano la Upimaji wa Afya Bure kwa Wananchi wa Dar es salaam, ambapo amewasihi Wananchi kujiwekea utaratibu wa kupima Afya zao mara kwa mara.

Hadi kufikia majira ya Mchana zaidi ya Wananchi 11,000 walikuwa tayari wamepimwa afya zao, Makonda amesema lengo ni kuhakikisha Wananchi wote zaidi ya 20,000 waliohudhuria wanapimwa na watakaobainika kuwa na matatizo ya kiafya Wanapatiwa Matibabu.

Makonda amewashukuru Madaktari,Wauguzi,Askari Polisi, Vyombo vya Habari,Watu wa Usafi na Wadau wote waliojitoa kumuunga mkono hadi kufanikisha zoezi hilo.

Amesema kuwa Zoezi hilo la Siku tano limefanikiwa kwa 100% huku likigharimu kiasi cha zaidi ya Shilling Billion Moja ikihusisha Vipimo,Matibabu,Vyakula, Vinywaji ambapo gharama zote hizo zimegharamiwa na Wadau wa Maendeleo waliojitolea kumuunga mkono RC Makonda

Aidha RC Makonda amewapongeza Wananchi wote waliojitokeza na kuchangia Damu kwakuwa kiasi cha Damu walizochangia zitakwenda kuokoa maisha ya Wagonjwa.

Upimaji wa Afya ulihusisha Magonjwa yote ikiwemo Saratani, Kisukari, Presha, Macho, Homa ya Ini na Ugonjwa wa Moyo ikihusisha Madaktari bingwa na Wauguzi zaidi ya 300 kutoka Hospital za Umma, Jeshi na za Watu Binafsi.

No comments:

Post a Comment