Breaking




Tuesday, 3 October 2017

KESI YA NAIBU WAZIRI WA FEDHA YAPIGWA KALENDA


SUNGO BLOG

KESI ya Naibu Waziri wa Fedha wa zamani, Adam Malima na dereva wake, RamadhanMohammed, ya kuzuia Polisi kutekelezamajukumu yao na kushambuliaimeahirishwahadi Novemba Mosi mwaka huu.

Kesi hiyo iliyopo katika Mahakama ya HakimuMkazi Kisutuimeahirishwa baada ya upandewa mashtaka kuieleza mahakama hiyo kuwashahidi aliyetakiwa kutoa ushahidi hakupatamwaliko kwa wakati licha ya kuwepo kwashahidi mwingine mahakamani hapo.

Wakili wa Serikali, Patrick Mwitaakisaidianana Glory Mwendaalidai Mahakamani hapombele ya Hakimu Mkazi MkuuRespiciusMwijagekuwa kesi hiyo ilikuja kwa ajili yakuendelea na ushahidi na tayari walikuwa nashahidi Mwita Joseph, lakini kutokana na asiliya kesi hiloaliyepaswa kutoa ushahidialitakiwa kuwa Daktari Mchwempaka kabla ya Joseph.

Kutokana na maelezo hayoHakimu MkaziMkuuMwijage aliahirisha kesi hiyo hadiNovemba Mosi mwaka huu itakapoendelea naushahidi.

Katika hati ya mashtakaMalima anadaiwakuwa Mei 15, mwaka huu katika eneo la Masaki kwa makusudi alimzuia ofisa wa polisi mwenye namba  H.7818 PC Abdul kufanya kazi yake halali wakati alipokuwa akimkamata kwa kupaki vibaya gari lake alimshambulia na kumsababishia maumivu

No comments:

Post a Comment