Breaking




Sunday 2 July 2017

Tanzania utinga nusu fainali cosafa


Timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars baada ya kufanikiwa kuingia hatua ya robo fainali ya michuano ya COSAFA inayoendelea nchini Afrika Kusini, Jumapili ya July 2 ilicheza mchezo wake wa robo fainali ya michuano hiyo dhidi ya timu ya taifa ya Afrika Kusini Bafana Bafana ambao ni wenyeji.

Tanzania ambayo ilikuwa Kundi A na timu za Mauritius, Angola na Malawi, ilifanikiwa kutinga hatua ya robo fainali baada ya kumaliza kinara wa Kundi A ikiwa na point tano sawa na Angola lakini ilifuzu kwa tofauti ya magoli ya kufunga na kufungwa.

Good news ikufikie kuwa Tanzania inafuzu kucheza hatua ya nusu fainali ya michuano ya COSAFA kwa kuifunga Afrika Kusini ambao ndio timu mwenyeji kwa goli 1-0, goli likifungwa na Elias Maguli dakika ya 17 ya mchezo, Maguli pia ndio amefanikiwa kuwa mchezaji bora wa mechi.

No comments:

Post a Comment