Breaking




Wednesday, 13 September 2017

TOGO: MAANDAMANO YAMESABABISHA WATU 180 KUPOTEA

Sungo blog

Watu zaidi ya 180 wameripotiwa kupotea kufuatia maandamano yaliofanyika nchini Togo dhidi ya serikali.

Upinzani nchini Togo uliandaa maandamano ambayo yalikuwa na lengo la kupinga utawala wa Faure Gnassingbe.

Maandamano yalifanyika katika mji wa Lome na miji tofauti nchini Togo.

Serikali kwa upande wake ilitangaza kuwa waandamanaji 80 walikamatwa na Polisi.

Waandamanaji walisikika wakitoa kauli za kukashifu utawa na kulaani katika kubadilishwa na kusema kuwa ardhi ya Togo sio milki ya Familia.

No comments:

Post a Comment