Breaking




Wednesday 4 October 2017

WOLPER AJIBU TUHUMA ZA KUACHANA NA BOYFRIEND WAKE

Sungo blog

  

Msanii wa filamu nchini, Jacquline Wolper ametolea ufafanuzi kuhusiana na uhusiano wake na Brown ambaye ameonekana kumunfollow Instagram na hivyo kuzuka tetesi kuwa wameachana. Hatua hiyo imekuja siku mbili tu baada ya mrembo huyo kuhudhuria birthday party ya Diamond ambapo pia ex wake Harmonize alikuwepo.

“Mimi na Brown tupo sawa tu jamani,” Wolper ameiambia Dizzim Online. “Hakuna kitu chochote kibaya kinachoendelea kati yetu kama watu wanavyofikiria na hicho alichokifanya ni kitu cha kawaida tu jamani, so mashabiki waendelee kusupport kazi zangu kama kawaida.”

Hata hivyo Wolper hajafafanua kwanini amefuta picha na video zote alizopost Instagram akiwa na Brown.

No comments:

Post a Comment