sungo blog
Umoja wa Ulaya (EU) umeipatia serikali ya Tanzania msaada wa Euro Milioni 4.5 (Tsh. 12 Bilioni) ili kufanikisha miradi mikubwamitatu ya sekta ya kilimo ambayoinatekelezwa kupitia Mpango wa KuendelezaKilimo Ukanda wa Kusini mwa Tanzania (SAGCOT).
Miradi hiyo itatekelezwa katika mikoa yaIringa, Morogoro ambapo itafanyika miradimiwili.
Akizungumza kuhusu msaada huo, NaibuWaziri wa Kilimo, Mary Mwanjelwa alisemamsaada huo utasaidia wakulima wadogokuboresha kilimo chao na kuwa chakibiashara zaidi kuliko sasa.
Mwanjelwa alisema pamoja na kuwanufaishawakulima, pia kama nchi itanufaika kutokanana biashara itakayokuwa ikifanyika jamboambalo litasaidia uchumi wa nchi kukua.
“Wamekusudia kufufua kilimo cha kisasa, kilimo bora ili Watanzania wanufaike na kilimo kwa kuwa na soko. Faida yake ni upatikanaji wa chakula, lishe na biashara na mwisho wa siku wananchi wote wanufaike,” alisema Mwanjelwa.
Kwa upande wa Balozi wa Umoja wa Ulaya hapa nchini, Roeland Van de Geer alisema EU imedhamiia kusaidia mirad mingi hapa nchini katika sekta ya chakula ili kuhakikisha kuwa jamii ya Tanzania inakuwa na chakula cha kutosha.






No comments:
Post a Comment