Breaking




Friday, 23 February 2018

WAZIRI NDALICHAKO AAHIDI KUMSOMESHA MDOGO WA MAREHEMU AKWILINA HADI CHUO KIKUU

Sungo blog


Waziri wa Elimu, Profesa Joyce Ndalichako ameahidi kumsomesha mdogo wake Akwilina Akwilini, Angela Akwilini ambaye kwa sasa anasoma kidato cha tatu.

Akizungumza leo Februari 23, 2018 baada ya mazishi ya Akwilina aliyeuawa kwa kupigwa risasi Februari 16, 2018 eneo la Mkwajuni jijini Dar es Salaam, Profesa Ndalichako amesema atamsomesha Angela hadi Chuo Kikuu. 

 “Binti huyu ambaye tumempumzisha kwenye nyumba yake ya milele alikuwa anapambana katika kusaka elimu ili aweze kuikwamua familia yake nimesikitika pia kuona kwamba pamoja na fedha zile ambazo Akwelina alikuwa anapata kwa ajili ya yeye kujikimu lakini alikuwa anatumia fedha hizo hizo kumsaidia mdogo wake Angela ambaye yupo kidato cha tatu naomba nisema kwamba huyo binti Angela nitamchukua kwa sababu natambua na kuthamini elimu hivyo nitahakikisha kwamba namsomesha mpaka uwezo wake na ndoto zake zitakapofikia,”amesema Prof. Ndalichako wakati wa kuuaga mwili wa Akwelina.

No comments:

Post a Comment