Breaking




Saturday, 26 August 2017

ALICHOZUNGUMZA MASAU BWIRE,MSEMAJI WA RUVU SHOOTING BAADA YA KUFUNGWA GOLI 7-0 NA SIMBA

Sungo blog


 

Msemaji machachari wa klabu ya Ruvu Shooting,Masau Bwire amesema ushindi walioupata Simba wa goli 7-0 dhidi ya timu yake ya Ruvu Shooting leo ni miujiza.

Masau Bwire ameyasema hayo  wakati akihojiwa na kipindi cha michezo cha E-spots  kinachorushwa na EFM.

Maasau amesema ushindi waliopata simba ni  miujiza kama miujiza mingine ambayo mwezimungu anaamua kuileta,na sio uwezo wa Simba.

"Ile ni miujiza tu kama ilivo mingine, hakuna goli lolote la kiufundi ambalo simba wamefunga" Aliseme Masau Bwire

Simba wameifunga Ruvu shooting magoli saba kwa sifuri ,magoli yaliyofungwa na Emannuel okwi(4),Kichuya (1),Erasto Nyoni (1) na Juma Luizio (1)

No comments:

Post a Comment