Breaking




Friday 7 July 2017

TCRA WATOA ONYO LA MWISHO KWA MITANDAO YA SIMU KUHUSU MATANGAZO

Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, Mhandisi James Kulaba 

Dar es Salaam. Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imezitaka kampuni za simu za mikononi kusitisha matangazo wakati wateja wanapiga simu vinginevyo wataadhibiwa.

Akizungumza jijini hapa leo Alhamisi, Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, Mhandisi James Kulaba amesema kumekuwa na malalamiko mengi kutoka kwa wateja kuwa wanapopiga simu huanza kusikiliza matangazo ya kampuni hizo badala ya watu wanaowapigia.

Amesema sheria na kanuni za kumlinda mtumiaji wa huduma za mwaka 2011 zinataka watoa huduma kutoa matangazo wakati wa kumjibu mteja anapoulizia salio la muda wa maongezi.

Kulaba amesema watoa huduma wanaweza kutangaza wakati mteja anapopokea taarifa baada ya kuongeza salio na anapoingia katika orodha ya huduma za kampuni husika.

"Kanuni zipo za kuzuia matangazo kiholela lakini kampuni za simu zinakiuka sasa kuanzia leo sitisheni au mtapambana na adhabu,"amesema.

Kulaba amesema wateja wameonyesha hisia ya kukerwa na utitiri wa matangazo yasiyozingatia kanuni za mamlaka hiyo.

Kuhusu adhabu, Kilaba amesema kuna aina nyingi za adhabu zinazoweza kutolewa ikiwemo kuzifungia kabisa zisifanye kazi nchini

No comments:

Post a Comment