Breaking




Friday 7 July 2017

UJIO A EVERTON WALETA NEEMA NCHINI

 Mkurugenzi wa Utawala wa SportPesa, Abbas Tarimba.

Kampuni ya Sportpesa nchini umesema muda wowote kutokea sasa ugeni wa kwanza kutoka timu ya Everton utawasili kwa kuwa maandalizi yote yamekamilika. 

 

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi wa Utawala wa SportPesa, Abbas Tarimba kwa kusema ujio wa Everton hivi sasa ni uhakika bila ya kuwa na shaka yeyote huku akidai kiungo na nahodha wa zamani wa timu hiyo, Leon Osman kuwa anatarajiwa kuanza kufika Julai 8 kabla ya kikosi chote kitakachominyana na Gor Mahia ya kutokea Kenya.

Mbali na hilo, Tarimba amewaambia wadau wa soka kuwa siku hiyo kutakuwa na kila aina ya burudani kutoka kwa magwiji hao tofauti na mpira wa uwanjani dakika 90.

"Kuna vitu vingi vitafanyika baada ya mchezo huo kwa maana Everton watazunguka na baiskeli Jijini Dar es Salaam ili kuweza kuutukuza na kuutangaza utalii wa Tanzania lakini vile vile Julai 8 na 9 Leon Osman atachukuliwa na Bodi ya Utalii kupelekwa hifadhi ya Ngorongoro. Kwa kweli mambo ni makubwa sana yatakayo kuwepo kwa siku hiyo", amesema Tarimba.

Pamoja na hayo, Tarimba amesema tiketi za kuweza kuhudhuria mtanange huo ambapo bei ya chini imepangwa kuwa shilingi elfu 3 huku VIP ikiwa ni shilingi elfu 8.

"Kuna tiketi elfu 8 zitakazotolewa bure kwa wachezaji wetu wa 'Sport Betting' kwa upande huu wa Sportpesa pamoja na watakao kwenda kuangalia mpira huku wakiwa wamevaa na jezi za Sportpesa, miongoni mwao watapata tiketi hizi za mualiko wa bure na watakaa VIP. Ni kitu kikubwa ambacho kitafanya watanzania walio wengi kuhudhuria mechi hii”, amesisitiza Tarimba

No comments:

Post a Comment