Breaking




Tuesday 4 July 2017

Mtandao wa Biashara ya Ukahaba wavunjwa

Baadhi ya watu waliowahi kufungwa kutokana na kujihusisha na Mtandao wa biashara haramu za binadamu
Image captionBaadhi ya watu waliowahi kufungwa kutokana na kujihusisha na Mtandao wa biashara haramu za binadamu
Polisi nchini Hispania wamesema wanawake 13 waliokuwa wamelazimishwa kufanya kazi za ukahaba katika kituo kimoja cha utalii mjini Puerto Banus wameachiliwa huru.
Wanawake hao wanadhaniwa kuwa waliletwa katika eneo hilo, kutoka nchini Bulgaria.
Polisi katika nchi zote mbili wamewakamata watu 34, wanaotuhumiwa kuwatishia wanawake hao na familia zao kuwafanyia fujo iwapo watakataaa kufanya kazi hiyo.
Kukamatwa kwa watu hao, kumekuja takriban miaka mitatu baada ya polisi kutahadharishwa kuhusiana na mtandao wa Ukahaba na wanawake ambaye alikwepa mtego wa kuingizwa katika biashara hiyo.
Polisi wanasema wanawake hao pia wamekuwa wakitumika kuibia wateja wake hao na kwamba baadhi yao walikuwa wakitumia madawa ya kulevya.

No comments:

Post a Comment